PaPi Clever & Dorcas - Mwokozi Wetu Lyrics

Contents:

Mwokozi Wetu Lyrics

Mwokozi wetu anatupa furaha duniani
Atuongoza kwa neema na anatushibisha
Tazama, yupo pamoja nasi, neema haitaisha kamwe
Haleluya, haleluya, haleluya
Amina
Tazama, yupo pamoja nasi, neema haitaisha kamwe
Haleluya, haleluya, haleluya
Amina

Ni vema kumpenda Mungu aliyetukomboa
Vizuri kuwa mtu wake, sitapotea kamwe
Furaha yetu itabakia, ikiwa vyote vingetoweka
Haleluya, haleluya, haleluya
Aminia
Furaha yetu itabakia, ikiwa vyote vingetoweka
Haleluya, haleluya, haleluya
Aminia

Ikiwa giza mara nyingi, na jua likifichwa
Na tukijaribiwa huku twajuwa ni kwa mda
Mbinguni hatutaona kamwe huzuni wala machozi tena
Haleluya, haleluya, haleluya
Aminia
Mbinguni hatutaona kamwe huzuni wala machozi tena
Haleluya, haleluya, haleluya
Aminia

Na tusisumbukie tena chakula wala nyumba
Maana vyote twavipata kwa ne’ma yake Mungu
Njiani yote atuongoza aichukuwa mizingo yetu
Haleluya, haleluya, haleluya
Aminia
Njiani yote atuongoza aichukuwa mizingo yetu
Haleluya, haleluya, haleluya
Aminia

Ikiwa vema huku chini kutegemea Yesu
Furaha gani huko juu kuona uso wake
Tutaiona furaha tele, na utukufu hautaisha
Haleluya, haleluya, haleluya
Aminia
Tutaiona furaha tele, na utukufu hautaisha
Haleluya, haleluya, haleluya
Aminia


PaPi Clever & Dorcas Songs

Related Songs